Showing posts with label newz ogo. Show all posts
Showing posts with label newz ogo. Show all posts

Thursday, 11 June 2009

BAJETI YA TANZANIA 2009/10 YASOMWA LEO BUNGENI

Bajeti ni Tegemezi kwa 30%
Taasisi za kidini kuanza kulipa kodi
Walevi na wavuta sigara wazidi kubanwa
Wizara ya Elimu yapewa kipaumbele
Matumizi ya serikali yazidi kwa 30%
Mapato hayaridhishi
Wafugaji wasahauliwa
Zanzibar yapata 4.5% ya bajeti
Wananchi wajiuliza, Je, Kweli Itawasaidia
Ni Nini maoni ya wananchi na viongozi wengine kuhusu bajeti hii?


Tulisubiri tangu zamani,tangu tukisikia sera za maandalizi ya bajeti ya mwaka huu wa 2009/10 ambapo mambo mengi yalifanywa na serikali ili kuhakikisha kwamba bajeti inakwenda sambamba na matakwa ya Watanzania wote, wengi wao wakiwa masikini.Bajeti hii imesomwa leo ikiwa imeatanguliwa na hotuba ya Rais wa Jamhuri wa Muungano hapo jana alipokuwa akizungumza na wazee wa Dodoma pia watanzania wote katika ukumbi wa Kilimani ambapo jambo kubwa alilozungumza ni kuhusu madhara ya mtikisiko wa uchumi duniani.Kiufupi ni kwamba hotuba hiyo iliwavutia wengi.
Sasa turudi katika suala letu la siku ya leo,suala nyeti ambapo leo mida ya saa kumi jioni tumemshuhudia Waziri wa Uchumi Tanzania Mhe.Mustapha Haidi Mkulo akifungua mkoba na kutusomea bajeti hiyo.Tuache longolongo shuhudia mwenyewe hapo chini angalau muktasari au wazungu wanasema 'summary' ya bajeti hiyo

SEKTA -MIUNDOMBINU Sh.1.1 Bilioni Ikiwa ni ongezeko la 12%
-KILIMO Sh.667.0 Bilioni ongezeko la 30%
-MAJI/UMWAGILIAJI Sh.347.3 Bilioni ongezeko la 50%
-NISHATI/MADINI Sh.285.5 Bilioni pungufu kwa -24.6
-ELIMU Sh.1.74 Trilioni ongezeko la 22%
-AFYA Sh.963.0 Bilioni ongezeko la 5.7%

MAELEZO MENGINEYO
MAPATO YA NDANI NI SH.TRILIONI 5.1
MATUMIZI YA SERIKALI NI SH.9.5 TRILIONI-Ikiwa ni ongezeko la 30%
KUDHIBITI KUYUMBA KWA UCHUMI SH.1.7 TRILIONI
WAHISANI SH.3.8 TRILIONI
BAJETI TEGEMEZI KWA 34%
MENGINEYO 1.2 TRILIONI

MAONI YA WATU MBALIMBALI KUHUSU BAJETI HII
Profesa Ibrahim Lipumba "uwazi unahitajika katika katika ulipaji wa makampuni,tusije kupata EPA ya pili manake bajeti inaweza kupangwa halafu utekelezaji ukawa sifuri". Pia Prof.Lipumba aliongeza kwamba bajeti hii haijamzingatia mtanzania wa kawaida yaani masikini, "masikini hawafaidiki na bajeti hii badala yake mabenki ndo yatakayofaidika na bajeti hii".
Said Kubenea "Ni kweli fedha zimetengwa lakini hatuna uhakika na utekelezaji huko mawizarani,yanweza kuzaliwa 'Marichmondi'mengine huko na yakalipwa fedha hizi".
Ole Sendeka-Mbunge wa Simanjiro "inashangaza kuona kwamba bajeti imekumbuka wakulima tu,wafugaji je? Bajeti hii imewasahau kabisa wafugaji wa kawaida kama wa kule Simanjiro watafaidika nini na bajeti hii? Halafu pia inashangaza kuona hata taasisi za kidini zinatozwa kodi ya VAT,hili limetushitua wengi sana".
John Cheyo-Mbunge wa Bariadi-"suala la madini limefumbiwa macho kabisa,tuliunda tume tukatoa mapendekezo lakini hakuna hata moja lililofanyiwa kazi.Wakubwa katika migodi wameendelea kulindwa na kuogopwa na bajeti hii".
Aidha katika hali ya kushangaza taasisi za dini ambazo zimekuwa zikitoa mchango mkubwa sana katika maendeleo ya nchi eti! nazo zitaanza kutozwa kodi katika baadhi ya huduma 'isipokuwa huduma za kiroho'.Hata hivyo jambo hili limewakera wengi na kushangazwa na kauli hii katika bajeti ya mwaka huu.Wengi hawajalipokea suala hili katika mtazamo chanya na wanasubiri kuona Bunge litachukua hatua gani wakati wa kujadili na kuiptisha bajeti hii wiki ijayo.Ikiwa ni hali nyingine ya kushangaza,waziri Mkulo amesema kwamba msukumo umewekwa zaidi katika kilimo wakati bajeti inaonesha kwamba ni sh.667.0 Bilioni tu zilizoelekezwa katika wizara hiyo.
Haya sasa wewe je,mwananchi wa kawaida una maoni gani kuhusiana na bajeti hii?
Je,kweli unaona itakusaidia?
Tafadhali tupe maoni yako.

Na Frank Joram
Mwandishi wa makala hii
11/06/2009

Friday, 29 May 2009

Lil Wayne ,The Carter

Lil Wayne also known as "Weezy Baby" is one of the most talented, controversial and famous rappers of our time. His incredible lyrics, rhythmic songs and the unique musical versions that he brings to hip-hop and rap lovers are some of the things that characterize him and his awesome work. Much of the controversy which surrounds him is based upon the history that he has chosen to brand his body with, as you'll see below some people completely dislike this style and yet love his music which is directly reflected on the number of sales generated by his most recent album.

Lil Wayne's Tattoos





























Lil Wayne Awards

Here you can view a complete and full list of all the awards Lil Wayne has won since the start of his career:

Award Song/Album Category

Grammy Awards 2009 Lollipop -Best Rap Song
Grammy Awards 2009 A Milli -Best Rap Solo Performance
Grammy Awards 2009 Swagga Like Us -Best Rap Performance By A Duo Or Group
Grammy Awards 2009 Tha Carter III -Best Rap Album
BET Hip Hop Awards 2008 Lollipop -Best Ringtone Of The Year
BET Hip Hop Awards 2008 I'm So Hood (Remix) -Best Hip-Hop Collabo
BET Hip Hop Awards 2008 ~ -MVP Of The Year
BET Hip Hop Awards 2008 ~ -Lyricist Of The Year
BET Hip Hop Awards 2008 Tha Carter III -CD Of The Year
BET Hip Hop Awards 2008 A Milli -People's Champ
BET Hip Hop Awards 2008 A Milli -Track Of The Year
MTV Europe Music Awards 2008 ~ -Artists Choice
MTV Video Music Awards 2008 Lollipop -Best Hip-Hop Video
Ozone Awards 2008 ~ -Best Rap Artist
Ozone Awards 2008 ~ -Best Lyricist
BET Awards 2008 Lollipop -Viewer's Choice Award
Ozone Awards 2007 We Takin' Over -Best Video
Ozone Awards 2007 ~ -Best Lyricist
Ozone Awards 2007 ~ -Best Male Rap Artist
Ozone Awards 2007 ~ -Mixtape Monster Award
Vibe Music Awards 2007 ~ -Best Rapper
BET Awards 2007 Stuntin' Like My Daddy -Viewer's Choice Award
BET Hip Hop Awards 2007 Stuntin' Like My Daddy Attel -People's Choice Award


Lil Wayne Nominations:

Below you can view a complete and full list of all the awards Lil Wayne has been nominated for since the start of his career:

Award Song/Mixtape/Album Category

Grammy Awards 2009 Tha Carter III -Album Of The Year
Grammy Awards 2009 Swagga Like Us -Best Rap Song
Grammy Awards 2009 Mr. Carter -Best Rap Performance By A Duo Or Group
Grammy Awards 2009 Got Money -Best Rap/Sung Collaboration
MTV Europe Music Awards 2008 ~ -Urban Artists
BET Hip Hop Awards 2008 Lollipop -Best Hip-Hop Video
BET Hip Hop Awards 2008 ~ -Hustler Of The Year
BET Hip Hop Awards 2008 Lollipop -Track Of The Year
BET Hip Hop Awards 2008 I'm So Hood (Remix) -Best Hip-Hop Video
BET Hip Hop Awards 2008 ~ -Best Live Performer
American Music Awards 2008 ~ -Artist Of The Year
American Music Awards 2008 Tha Carter III -Favorite Hip-Hop/Rap Album
American Music Awards 2008 ~ -Favorite Male Hip-Hop/Rap Artist
Ozone Awards 2008 Duffle Bag Boy -Club Banger Of The Year
Ozone Awards 2008 Lollipop -Best Video
Ozone Awards 2008 Lollipop -Club Banger Of The Year
Ozone Awards 2008 ~ -Mixtape Monster Award
Ozone Awards 2008 ~ Trillest Award
Ozone Awards 2008 ~ Best Rap Group - Birdman
Ozone Awards 2008 ~ TJ's DJ's Hustler Award
Grammy Awards 2008 Make It Rain -Best Rap Performance By A Duo
BET Awards 2008 I'm So Hood (Remix) -Best Collaboration
Teen Choice Awards 2008 ~ -Choice Rap Artist
BET Awards 2008 ~ -Best Male Hip-Hop Artist
MTV Video Music Awards 2008 Lollipop -Best Male Video
BET Hip Hop Awards 2007 ~ -Lyricist of the Year
BET Awards 2007 ~ -Best Male Hip-Hop Artist
Vibe Music Awards 2007 Da Drought 3 -Best Mixtape Of The Year
BET Hip Hop Awards 2007 ~ -Best Live Performance
Ozone Awards 2007 You -Best Rap/R&B Collaboration
BET Hip Hop Awards 2007 Stuntin' Like My Daddy -Best Hip Hop Collabo
Vibe Music Awards 2007 We Takin' Over -Coolest Collabo
MTV Video Music Awards 2006 -Fireman MTV2 Award
Grammy Awards 2006 Soldier -Best Rap/Sung Collaboration
MTV Video Music Awards 2005 Soldier -Best Group Video
Vibe Music Awards 2005 Soldier -Coolest Callabo
BET Awards 2005 Soldier -Best Collaboration
Source Awards 2000 ~ -Best New Artist

Thursday, 14 May 2009

Mwanahalisi Kumlipa Rostam Shilingi Bilioni Tatu!!!!


Mahakama kuu kanda ya Dar es salaam jana iliamuru
wahariri pamoja na waandishi wa habari kumlipa Bwana
Rostam Aziz,mbunge wa Igunga kiasi cha shilingi
bilioni tatu(3bil.) ikiwa ni fidia kwa chombo hicho
cha habari kumdhalilisha bwana Rostam Azizi kwa
kuchapisha katika gazeti la Mwanahalisi habari isiyo
ya kweli na hivyo kumshushia heshima bwana Rostam Aziz.
Mwanahalisi ilichapisha habari iliyodai kwamba Rostam
Aziz ni fisadi na ni mtu mchafu katika jamii. Jaji
aliyesimamia kesi hiyo na kutoa maamuzi ni Jaji Robert
Makaramba ambaye alisema amefikia maamuzi hayo baada
ya gazeti la mwanahalisi kushindwa kutokea mahakamani kutoa ushahidi katika kutoa utetezi wake.Hata hivyo mwanasheria
wa gazeti la Mwanahalisi,Mtanzania Halisi bwana Marando
amesema kwamba tayari wameanza kuchukua hatua za awali kwa
ajili ya kukata rufaa.